HII HAPA NDIO IDADI YAWATU WENYE SIMU | ISOME HAPA>>INASHTUA

BOFYA HAPA UJISHINDIE ZAWADI YA GARI KILA SIKU=> CLICK AND WIN A CAR=> Click Here=>

Msemaji wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prisca Ulomo aliyasema hayo jana jijini Dar es Salam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Kanuni mpya za Huduma za Ziada za mwaka 2015 za Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta ya mwaka 2010.
Aidha, alisema watumiaji wa mfumo wa intaneti nao wameongezeka kutoka milioni 3.56 mwaka 2008 hadi milioni 11.34 mwaka 2014.
Alisema mafanikio hayo, yamerahisisha kutoa na kupata huduma kwa haraka na kwa wakati na wananchi hawalazimiki tena kusafiri sambamba na kupunguza urasimu katika huduma za kutuma na kupokea fedha.
“Huduma hii imesaidia mengi ikiwemo kulipia ankara za maji, umeme, ada na ukusanyaji wa mapato ambapo takwimu zinaonesha kwamba kuna watumiaji 12,330,962 wa miamala ya kifedha na ununuzi wa huduma na bidhaa kwa kutumia miamala ya kibenki,” alisema.
Alisema mafanikio hayo, pia yameleta changamoto kwenye sekta na katika jamii, ikiwemo utoaji wa huduma za ziada kwa watumiaji wa huduma za ziada bila kuwa na utaratibu unaoeleweka kati ya mtoa huduma na mpokea huduma au mlaji.
“Baada ya kujitokeza kwa changamoto katika utoaji wa huduma za ziada, serikali kupitia Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia ilitunga kanuni mpya za Huduma za Ziada za Mwaka 2015 ambayo tayari imeshaanza kutumika,” alisema.
Alisema lengo kuu la kanuni hizo ni kuweka utaratibu mahususi, unaoeleweka wa utoaji na upokeaji wa huduma za ziada, ambazo ni huduma za mawasiliano za kielektroniki zinazotolewa kupitia mitandao zaidi ya huduma za msingi za mawasiliano, mfano kupokea ujumbe

FUNGUA HAPA KUSHINDA ZAWADI KEMKEM=>CLICK HERE TO WIN => Click Here=>

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright MTANGANJIA Published.. Blogger Templates
Back To Top