DUH YANGA MASTREIKA 8 !! KWELI MMEAMUA

BOFYA HAPA UJISHINDIE ZAWADI YA GARI KILA SIKU=> CLICK AND WIN A CAR=> Click Here=>

SIMBA-YANGA-12.jpgWachezaji wa Yanga wakishangilia.
Nicodemus Jonas, Dar es Salaam
YANGA imeizidi kete Simba katika utitiri wa washambuliaji baada ya usajili wa nyota wawili kwa mpigo; Paul Nonga na Issofou Boubacar ‘Garba’ ambao umeifanya kuwa na jumla ya washambuliaji nane, mmoja zaidi ya watani wao.
Busunguuu.jpgWakati wadau wa soka wakijadili umuhimu wa Nonga katika jeshi lililosheheni washambuliaji wakali, Yanga wamekuja juu na kusema kuwa na ingewezekana wangeendelea kuongeza wengine kwani wanataka kuwa na kikosi kipana zaidi.
Safu ya mbele inaundwa na; Amissi Tambwe, Donald Ngoma, Garba, Nonga, Matheo Simon na Malim Busungu, wakati huohuo kuna viungo washambuliaji Geoffrey Mwashuiya na Simon Msuva ambao pia wanao uwezo wa kufunga.
Akifafanua kiufundi zaidi, Kocha Msaidizi wa Yanga, Juma Mwambusi amesema kuwa, benchi lilifikia uamuzi huo kutokana na wingi wa mashindano yanayowakabili, ikiwemo Ligi ya Mabingwa Afrika (Caf).
“Ukiangalia tuna michuano mingi ambayo inatulazimu kuwa na kikosi kipana zaidi. Caf, ligi kuu, Kombe la FA na hapohapo Mapinduzi inatusubiri siku chache zijazo.
YANGA-MTIBWA-11.jpg“Hivyo kuna kila sababu ya kuwa na kikosi kipana, siyo kuwategemea wachezaji walewale (Donald) Ngoma na (Amissi) Tambwe, wakiumia je?
“Hivyo lazima uwe na kikosi kipana ili kama ni kasi ya kushambulia kusionekane pengo michuano kwa michuano,” alisema Mwambusi.
FUNGUA HAPA KUSHINDA ZAWADI KEMKEM=>CLICK HERE TO WIN => Click Here=>

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright MTANGANJIA Published.. Blogger Templates
Back To Top